Mungu Wa Ajabu

Text
0
Kritiken
Leseprobe
Als gelesen kennzeichnen
Wie Sie das Buch nach dem Kauf lesen
Mungu Wa Ajabu
Schriftart:Kleiner AaGrößer Aa

Mungu wa Ajabu

Mungu ni mkuu na wa kutisha. Jina lake ni la Ajabu.

André CRONJE

Translated by Winnie Ngimor

Hakimiliki

Ina leseni kwa ajili ya uboreshaji binafsi na inaweza kutumika kwa ujenzi wa maadili na kutia motisha. Hakuna sehemu inayoweza kunakiliwa tena kwa faida au kuuza tena.

André Cronje © 2020 Hakimiliki

Sanaa ya Dhana na André

Heshima maalumu kwa King James.

Mwandishi

Andre ni mzaliwa wa Afrika Kusini mzao wa Huguenot anayeishi Paris, Ufaransa. Yeye ni msanii, mwandishi, na mmiliki wa duka mtandaoni la nguo za Kikristo. Kama mfinyanzi aumbavyo udongo wake, ndivyo anavyounda na kuboresha mawazo yake kuhusu mada anuwai, kwa sanaa ya dhana, na fasihi ya kinabii, akisisitiza maswala ya kijamii, kimaadili, na kiroho na nuru ya Yesu Kristo, ambaye alikufa na kufufuka, akisamehe dhambi, akiponya wagonjwa, na ni mtoaji wa uzima wa milele, kwa yeyote anayeamini na kubatizwa kwa jina lake.

https://andrecronje.me

Yaliyomo

Hakimiliki

Mwandishi

1. Wimbo wa Yesu

2. Ni Siku Nzuri

3. Msifuni Yah

4. Yesu Rafiki Yangu

5. Hakuna Kisichowezekana

6. Imba na Uombe

7. Yeye ni Mkuu Zaidi

8. Mungu Baba

9. Niko Peke Yangu

10. Tatu, Mbili, Moja

11. Kuishi kwa Imani

12. Mlima Songa!

13. Tumaini Tena

Baraka Kwako

1. Wimbo wa Yesu

Yesu wewe Ndiye wangu, Yesu wewe Ndiye unayeangaza, Yesu wewe ni, Shujaa wa Pekee, aliyetoka mbinguni na kunitenga, kwa ajili ya ufalme wako na utukufu wako, Bwana.

Yesu wewe Ndiye wangu, jua kali, nuru ya ulimwengu, angazia maisha yangu, na uangaze kupitia mimi, nuru gizani, ili wote waweze kuona, kuwa wewe Ndiye, mwana wa Pekee wa Mungu .

Yesu wewe Ndiye wangu, neno la Mungu, Imanueli, Mungu pamoja nasi, mwana wa binadamu, mtoto wa bikira na mwana wa Baba, Aliyetumwa kutoka mbinguni na ujumbe kwa kila mtu, mnyenyekevu na mpole uliwafundisha watu wote, geuka kutoka kwa dhambi na umgeukie Mungu, ukweli umekuja, ambao utakuweka huru.

Yesu wewe Ndiye wangu, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa wote, juu ya mabega yako utawala wa sheria. Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Hakuna mungu mwingine, hakuna jina lingine, Mtu wa huzuni uliponya maumivu yangu, kutoka msalabani hadi kwenye kaburi tupu, ulifufuka tena, jahanamu imeshindwa, Kristo amefufuka, nimezaliwa mara ya pili.

Yesu wewe Ndiye wangu, rafiki wa rafiki yangu mwenye dhambi, uliponya wagonjwa, na kusamehe uhalifu, ukibadilisha maji kuwa divai. Viziwi watasikia, na bubu watazungumza, vipofu wataona watu wenye ukoma wakitakaswa, wafu wakitembea mara nyingine tena.

Yesu wewe Ndiye wangu, neno la Mungu lililotabiriwa, mwana-kondoo wa Mungu atatolewa kafara, simba wa Yuda mfalme wa Wayahudi, mwenye nguvu, wa ajabu, mshauri, mfalme wa amani, tangu milele hata milele, Baba, mimi ni mtoto wako,

Yesu wewe Ndiye wangu, Yesu wewe Ndiye unayeangaza, Yesu wewe ni, Shujaa wa Pekee, aliyetoka mbinguni na kunitenga, kwa ajili ya ufalme wako na utukufu wako, ndiyo mfalme wangu, - haleluya usifiwe Yesu.

2. Ni Siku Nzuri

Ni siku nzuri ya kuimba sifa zako, ni siku nzuri iliyojaa upendo na neema. Ni siku nzuri kukujua, Mungu, Ni siku nzuri dhambi zangu zimeoshwa. Ni jambo zuri kusifu na kuimba, ndiyo, kukutawaza Bwana na mfalme. Ni siku nzuri na njia tunayojua.

Ni siku nzuri, ndio maana nakuja mapema kuomba. Ni siku nzuri nitakaa pamoja na Mungu. Ni siku nzuri iliyojaa jua na mvua ya thamani. Ni siku nzuri nakupa upendo wangu. Ni siku nzuri iliyojaa zawadi kutoka juu. Ni siku nzuri, wewe ni sababu yangu maneno hayatoshi.

Ee Mungu wangu, ni siku nzuri, Ee Mungu wangu njia ni nzuri jinsi gani. Ee Mungu wangu pamoja nawe nitakaa, Mungu Wangu maneno hayatoshi.

Ni siku nzuri, Mungu wangu, na njia zako pia. Wewe ndiye sababu ya kutabasamu nikifanya mengi zaidi, na wewe ndiye sababu yangu kuimba. Mfalme wangu mpendwa, kwani nilipopata njia yako, nilipata nyumba yangu, Ee Mungu wangu pamoja nawe nitakaa. Ee Mungu wangu, ni siku nzuri. Nitakufuata kupitia njia iliyonyooka na nyembamba.

Ee Mungu wangu, ni siku nzuri. Ninapokea upendo wako, zawadi kutoka juu. Ee Mungu wangu, ni siku nzuri ya kujaa upendo, amani, na furaha. Ni siku nzuri, Mungu wangu, ni siku nzuri kwa sababu upo katika mwendo wote.

Sie haben die kostenlose Leseprobe beendet. Möchten Sie mehr lesen?

Weitere Bücher von diesem Autor